Wednesday, 17 September 2014

KURASA ZA MAGAZETI LEO JUMATANO 17/09/2014 KWA HISANI YA MBEYA SPORT.BLOG

Kamakawaida mbeyasport inakupa uhuru wa kujua yaliyo jri leo kwenye magazeti na sio leo tuu nikila siku unakaribishwa kutembelea mtandao huu ilikupata habari za michezo udaku na kurasa za magazeti na habari zinazo tufikia hivi punde .
.

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

TEVEZ BADO MOTO, APIGA ZOTE MBILI JUVE IKIUA 2-0 ULAYA

 MABAO mawili ya mshambuliaji wa zamani wa Manchester United, Muargentina Carlos Tevez usiku huu yameipa ushindi wa 2-0 Juventus ya Italia katika mchezo wa makundi Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Tevez aliyewahi pia kuchezea Manchester City, alifunga bao moja kila kipindi dhidi ya Malmo FF ya Sweden katika dakika za 59 na 90 na kukipa mwanzo mzuri Kibibi Kizee cha Turin katika michuano hiyo mikubwa zaidi ya klabu barani Ulaya.
Wana fainali wa michuano ya msimu uliopita, Atletico Madrid wamepata kipigo cha ugenini kutoka kwa Olympiacos ya Ugiriki cha mabao 3-2.
Mabao ya wenyeji yamefungwa na Arthur Masuaku dakika ya 13, Ibrahim Affelay dakika ya 31 na Mitroglou dakika ya 74 wakati ya wageni yamefungwa na Mario Mandzukic dakika ya 38 na Griezmann dakika ya 87.
Carlos Tevez bado moto, amefunga zote mbili Juve ikiua 2-0 Ulaya

DANNY WELBECK 'ALIVYOWAKERA' ARSENAL JANA...

 MSHAMBULIAJI mpya wa Arsenal, Danny Welbeck jana alikuwa ana nafasi nzuri ya kuwa shujaa wa timu hiyo katika mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Borrusia Dortmund, lakini akashindwa kuitumia.

Mchezaji huyo aliyesajiliwa kwa Pauni Milioni 16 kutoka kwa wapinzani, Manchester United jana alienedelea kupewa nafasi katika kikosi cha kwanza cha The Gunners na kocha Arsene Wenger akionyesha alimsajili kwa sababu alimuamini, lakini akashindwa kuwafurahisha mashabiki.

Haamini macho yake; Mshambuliaji mpya wa Arsenal, Danny Welbeck akiwa amepiga magoti kwa masikitiko baada ya kupoteza nafasi nzuri ya kufunga kipindi cha kwanza jana

Muingereza huyo jana alipata nafasi tatu nzuri za kuifungia Arsenal mabao kuanzia mapema kipindi cha kwanza, lakini zote akashindwa kuzitumia, The Gunners wakichapwa mabao 2-0 na Dortmund ugenini.
Dhahiri Welbeck anahitaji kujiuliza mno baada ya mechi ya jana, kwani iwapo atarudia makosa aliyoyafanya katika mchezo huo, atajitengenezea mazingira ya kuondoka kwenye kikosi cha kwanza Gunners.
Welbeck stumbles at the back post under pressure and misses a chance to give Arsenal the lead
Mshambuliaji wa Arsenal, Danny Welbeck alipata nafasi nzuri ya kufunga hapa bao ambalo lingekuwa la kuongoza kwa Arsenal, lakini akakosa mpira ukimpita namna hii
Nyingine hii; Danny Welbeck akianguka chini na kumshuhudia kipa wa Dortmund, Roman Weidenfeller akienda upande mwingine wa lango na mpira ukitoka nje baada ya kushindwa kuunganishia nyavuni
Welbeck gets into another good shooting position late on but blazes the ball over the bar
Na hii tena; Welbeck akapata nafasi nyingine tena, lakini akapiga juu ya lango

WACHEZAJI MAN UNITED 'WAKESHA' KUANGALIA LIGI YA MABINGWA

 

KLABU ya Manchester United haimo kabia katika michuano ya Ulaya msimu huu baada ya kumaliza nafasi ya saba katika Ligi Kuu ya England msimu uliopita.
Pamoja na hayo, wachezaji wake wameendelea kuonyesha mapenzi na michano hiyo baada ya kukubakli kuchelewa kulala, ili waangalie mechi za Ligi ya Mabingwa. Kipa David de Gea na baadhi ya wachezaji wenzake jana walipoteza muda kwa ajili ya mechi za Ulaya.
Kipa huyo wa kimataifa wa Hispania, ameposti picha akiwa na wachezaji wenzake Marcos Rojo, Rafael, Antonio Valencia, Andreas Pereira, Anderson, Angel di Maria, Ander Herrera na Juan Mata wakipata chakula huku wanaangalia mechi za Ligi ya Mabingwa.
Mzuia michomo huyo wa zamani wa Atletico Madrid ameposti picha hiyo kwenye akaunti yake ya Twitter akiambatanisha na ujumbe: "Chakula cha usiku na timu"!.

Watazamaji; David de Gea akiwa na wachezaji wenzake Marcos Rojo, Rafael, Antonio Valencia, Andreas Pereira, Anderson, Angel di Maria, Ander Herrera na Juan Mata wakipata chakula cha usiku huku wakiangalia Ligi ya Mabingwa

Tuesday, 16 September 2014

Liverpool yarejea katika ligi kuu Ulaya


Liverpool yarejea katika ligi kuu Ulaya
Baada ya miaka 5 nje Liverpool leo wanawakaribisha timu ya Lugorets Razgrad,ya Bulgaria Anflied.
  •  

Wednesday, 3 September 2014

Jumatano, Septemba 3, 2014

     
Leo ni Jumatano tarehe 7 Dhilqaada 1435 Hijria, inayosadifiana na Septemba 3, 2014.
Siku kama ya leo miaka 96 iliyopita, Damascus mji mkongwe na wa kihistoria wa Kiislamu ulikaliwa kwa mabavu na vikosi vya majeshi ya Uingereza. Moja kati ya malengo makuu ya serikali za Ulaya Wakati wa Vita vya Pili vya Dunia ilikuwa kuusambaratisha utawala wa Othmania, lengo ambalo baadaye lilifanikiwa. Wakati utawala wa Othmania ulipokuwa ukisambaratika, maeneo yaliyokuwa chini ya utawala huo moja baada ya jingine yalidhibitiwa na Ufaransa na Uingereza, ambapo mji wa Damascus katika Syria ya leo, pia ulishambuliwa na katika siku kama ya leo ukakaliwa kwa mabavu.
katika siku kama ya leo miaka 71 iliyopita, mkataba wa kusalimu amri Italia katika Vita Vikuu vya Pili vya Dunia ulitiwa saini baina ya wawakilishi wa Italia na nchi waitifaki. Kwa mujibu wa mkataba huo, Waziri Mkuu wa Italia alikubali bila masharti kusalimu amri nchi yake na kwa utaratibu huo, mmoja wa waitifaki muhimu wa Ujerumani ya Kinazi katika vita hivyo, akawa ameondoka katika medani ya vita.
Na miaka 43 iliyopita, yaani tarehe 3 Septemba mwaka 1971, nchi ya Qatar ilipata uhuru toka kwa mkoloni Mwingereza. Katika karne ya 19, Qatar ilikuwa ikihesabiwa kuwa sehemu ya Peninsula ya Kiarabu. Baadaye nchi hiyo ikatawaliwa na kudhibitiwa na Ufalme wa Othmania. Hata hivyo kufuatia kudhoofika utawala huo, Qatar ambayo kuanzia mwaka 1882 na kuendelea kivitendo ilikuwa ikiendeshwa na Uingereza, mwaka 1916 nchi hiyo ya Kiarabu ikawa imetambuliwa rasmi kuwa koloni la Muingereza. Hadi mwaka 1971 Qatar ilikuwa bado inakoloniwa na Uingereza ambapo mwaka huo huo, kwa ushirikiano wa viongozi wa eneo la pambizoni mwa kusini mwa Ghuba ya Uajemi, likaundwa Shirikisho la Umoja wa Falme za Kiarabu. Hata hivyo mnamo Septemba mwaka huo huo, yaani 1971, Qatar ilijiondoa katika Shirikisho la Umoja wa Falme za Kiarabu na kujitangazia uhuru.

Barcelona yaanza LALIGA kwa makeke, Messi ang’ara

     
Timu ya soka ya Barcelona ya Uhispania imeanza msimu mpya wa ligi kuu ya soka nchini humo al-maarufu LALILGA kwa ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya timu ya Elche. Timu hiyo ambao kwa sasa inanolewa na mkufunzi Luis Enrique ikicheza katika uwanja wake wa nyumbani wa Camp Nou ilionekana ikiwa na sura nyingi ngeni baada ya kuwasajili makinda kadhaa akiwemo Munir El Haddadi mwenye umri wa miaka 18 ambaye anaonekana kuwa tishio katika safu ya ushambuliaji. Nyota wa timu hiyo Lionel Messi alipachika mabao 2 katika dakika za 42 na 63, huku bao la tatu likitiwa kimiani na kinda Munir El Haddadi katika dakika ya 46 ya mchezo. Mambo yalionekana yangewavurugikia Barcelona baada ya mlinzi wake Javier Mascherano kulimwa kadi nyekundu katika dakika ya 43 ya kipindi cha kwanza. Hata hivyo pengo la Mascherano halikuwa kikwazo kwa Barcelona kung’ara na kuibuka na ushindi katika mchezo huo. Katika mechi nyingine za ufunguzi zilizochezwa jana Celta de Vigo imeibamiza Getafe mabao 3-1, Villareal imeitandika Levante viboko viwili bila majibu, Granada imeipeleka mchakamchaka  Deportivo de la Coruna kwa kuifunga mabao 2-1, Malaga imeiadhibu Athletic bao 1 kwa yai, huku Sevilla na Valencia zikitoshana nguvu kwa kufungana bao 1-1, matokeoa ambayo yalitawala pia mchezo kati ya Almeria na Espanyol. Ligi hiyo itaendelea tena leo ambapo Real Madrid watamenyamana na Cordoba huku mabingwa watetezi Atletico Madrid wakiwa wageni wa Rayo Vallecano.