Wednesday, 17 September 2014
TEVEZ BADO MOTO, APIGA ZOTE MBILI JUVE IKIUA 2-0 ULAYA
MABAO mawili ya mshambuliaji wa zamani wa Manchester United, Muargentina Carlos Tevez usiku huu yameipa ushindi wa 2-0 Juventus ya Italia katika mchezo wa makundi Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Tevez aliyewahi pia kuchezea Manchester City, alifunga bao moja kila kipindi dhidi ya Malmo FF ya Sweden katika dakika za 59 na 90 na kukipa mwanzo mzuri Kibibi Kizee cha Turin katika michuano hiyo mikubwa zaidi ya klabu barani Ulaya.
Wana fainali wa michuano ya msimu uliopita, Atletico Madrid wamepata kipigo cha ugenini kutoka kwa Olympiacos ya Ugiriki cha mabao 3-2.
Mabao ya wenyeji yamefungwa na Arthur Masuaku dakika ya 13, Ibrahim Affelay dakika ya 31 na Mitroglou dakika ya 74 wakati ya wageni yamefungwa na Mario Mandzukic dakika ya 38 na Griezmann dakika ya 87.
Wana fainali wa michuano ya msimu uliopita, Atletico Madrid wamepata kipigo cha ugenini kutoka kwa Olympiacos ya Ugiriki cha mabao 3-2.
Mabao ya wenyeji yamefungwa na Arthur Masuaku dakika ya 13, Ibrahim Affelay dakika ya 31 na Mitroglou dakika ya 74 wakati ya wageni yamefungwa na Mario Mandzukic dakika ya 38 na Griezmann dakika ya 87.
![]() |
Carlos Tevez bado moto, amefunga zote mbili Juve ikiua 2-0 Ulaya |
DANNY WELBECK 'ALIVYOWAKERA' ARSENAL JANA...
MSHAMBULIAJI mpya wa Arsenal, Danny Welbeck jana alikuwa ana nafasi nzuri ya kuwa shujaa wa timu hiyo katika mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Borrusia Dortmund, lakini akashindwa kuitumia.
Mchezaji huyo aliyesajiliwa kwa Pauni Milioni 16 kutoka kwa wapinzani, Manchester United jana alienedelea kupewa nafasi katika kikosi cha kwanza cha The Gunners na kocha Arsene Wenger akionyesha alimsajili kwa sababu alimuamini, lakini akashindwa kuwafurahisha mashabiki.
Muingereza huyo jana alipata nafasi tatu nzuri za kuifungia Arsenal mabao kuanzia mapema kipindi cha kwanza, lakini zote akashindwa kuzitumia, The Gunners wakichapwa mabao 2-0 na Dortmund ugenini.
Dhahiri Welbeck anahitaji kujiuliza mno baada ya mechi ya jana, kwani iwapo atarudia makosa aliyoyafanya katika mchezo huo, atajitengenezea mazingira ya kuondoka kwenye kikosi cha kwanza Gunners.
Haamini macho yake; Mshambuliaji mpya wa Arsenal, Danny Welbeck akiwa amepiga magoti kwa masikitiko baada ya kupoteza nafasi nzuri ya kufunga kipindi cha kwanza jana
Dhahiri Welbeck anahitaji kujiuliza mno baada ya mechi ya jana, kwani iwapo atarudia makosa aliyoyafanya katika mchezo huo, atajitengenezea mazingira ya kuondoka kwenye kikosi cha kwanza Gunners.

Mshambuliaji wa Arsenal, Danny Welbeck alipata nafasi nzuri ya kufunga hapa bao ambalo lingekuwa la kuongoza kwa Arsenal, lakini akakosa mpira ukimpita namna hii

Nyingine hii; Danny Welbeck akianguka chini na kumshuhudia kipa wa Dortmund, Roman Weidenfeller akienda upande mwingine wa lango na mpira ukitoka nje baada ya kushindwa kuunganishia nyavuni
Na hii tena; Welbeck akapata nafasi nyingine tena, lakini akapiga juu ya lango
WACHEZAJI MAN UNITED 'WAKESHA' KUANGALIA LIGI YA MABINGWA
KLABU ya Manchester United haimo kabia katika michuano ya Ulaya msimu huu baada ya kumaliza nafasi ya saba katika Ligi Kuu ya England msimu uliopita.
Pamoja na hayo, wachezaji wake wameendelea kuonyesha mapenzi na michano hiyo baada ya kukubakli kuchelewa kulala, ili waangalie mechi za Ligi ya Mabingwa. Kipa David de Gea na baadhi ya wachezaji wenzake jana walipoteza muda kwa ajili ya mechi za Ulaya.
Kipa huyo wa kimataifa wa Hispania, ameposti picha akiwa na wachezaji wenzake Marcos Rojo, Rafael, Antonio Valencia, Andreas Pereira, Anderson, Angel di Maria, Ander Herrera na Juan Mata wakipata chakula huku wanaangalia mechi za Ligi ya Mabingwa.
Mzuia michomo huyo wa zamani wa Atletico Madrid ameposti picha hiyo kwenye akaunti yake ya Twitter akiambatanisha na ujumbe: "Chakula cha usiku na timu"!.
Tuesday, 16 September 2014
Liverpool yarejea katika ligi kuu Ulaya

Baada ya miaka 5 nje Liverpool leo wanawakaribisha timu ya Lugorets Razgrad,ya Bulgaria Anflied.
Wednesday, 3 September 2014
Jumatano, Septemba 3, 2014
Leo ni Jumatano tarehe 7 Dhilqaada 1435 Hijria, inayosadifiana na Septemba 3, 2014.
Siku kama ya leo miaka 96
iliyopita, Damascus mji mkongwe na wa kihistoria wa Kiislamu ulikaliwa
kwa mabavu na vikosi vya majeshi ya Uingereza. Moja kati ya malengo
makuu ya serikali za Ulaya Wakati wa Vita vya Pili vya Dunia ilikuwa
kuusambaratisha utawala wa Othmania, lengo ambalo baadaye lilifanikiwa.
Wakati utawala wa Othmania ulipokuwa ukisambaratika, maeneo yaliyokuwa
chini ya utawala huo moja baada ya jingine yalidhibitiwa na Ufaransa na
Uingereza, ambapo mji wa Damascus katika Syria ya leo, pia ulishambuliwa
na katika siku kama ya leo ukakaliwa kwa mabavu.
katika siku kama ya leo miaka
71 iliyopita, mkataba wa kusalimu amri Italia katika Vita Vikuu vya Pili
vya Dunia ulitiwa saini baina ya wawakilishi wa Italia na nchi
waitifaki. Kwa mujibu wa mkataba huo, Waziri Mkuu wa Italia alikubali
bila masharti kusalimu amri nchi yake na kwa utaratibu huo, mmoja wa
waitifaki muhimu wa Ujerumani ya Kinazi katika vita hivyo, akawa
ameondoka katika medani ya vita.
Na miaka 43 iliyopita, yaani
tarehe 3 Septemba mwaka 1971, nchi ya Qatar ilipata uhuru toka kwa
mkoloni Mwingereza. Katika karne ya 19, Qatar ilikuwa ikihesabiwa kuwa
sehemu ya Peninsula ya Kiarabu. Baadaye nchi hiyo ikatawaliwa na
kudhibitiwa na Ufalme wa Othmania. Hata hivyo kufuatia kudhoofika
utawala huo, Qatar ambayo kuanzia mwaka 1882 na kuendelea kivitendo
ilikuwa ikiendeshwa na Uingereza, mwaka 1916 nchi hiyo ya Kiarabu ikawa
imetambuliwa rasmi kuwa koloni la Muingereza. Hadi mwaka 1971 Qatar
ilikuwa bado inakoloniwa na Uingereza ambapo mwaka huo huo, kwa
ushirikiano wa viongozi wa eneo la pambizoni mwa kusini mwa Ghuba ya
Uajemi, likaundwa Shirikisho la Umoja wa Falme za Kiarabu. Hata hivyo
mnamo Septemba mwaka huo huo, yaani 1971, Qatar ilijiondoa katika
Shirikisho la Umoja wa Falme za Kiarabu na kujitangazia uhuru.
Barcelona yaanza LALIGA kwa makeke, Messi ang’ara
Iran yashinda dhahabu, fedha katika Mashindano ya Asia
Katika safu ya wanaspoti waliokuwa kwenye viti vya magurudumu katika mchezo huo wa kabadde, Thakur Vinod wa India alishinda dhahabu kwa kupata pointi 206. Muirani Shahabedin Basamtabar aliibuka wa pili kwa kupata pointi 149 na kujishindia medali ya fedha, kando na medali ya dhahabu aliyoishinda hapo awali. Asadullah wa Pakistan aliyeibuka wa tatu alijishindia medali ya shaba kwa kupata pointi 109.
Timu ya Iran imetwaa ubingwa wa mashindano hayo kwa kupata jumla ya pointi 39 ikifuatiwa na Pakistan na Tajikistan zilizopata pointi 33 na 31 mtawalia. India imeboronga katika mashindano hayo na kuvuta mkia.
Wanamichezo kutoka nchi hizo 4 za bara Asia wameshiriki duru ya kwanza ya Mashindano hayo ya Michezo ya Kunyoosha Viungo ya Bara Asia kwa Walemavu maarufu kama Parazurkhaneh yaliyofanyika katika ukumbi wa Abul Qasim Firdaus mjini Dushambe nchini Tajikistan.
Ligi Kuu ya Soka ya Iran
Klabu ya Esteqlal imeendelea kujikita kileleni mwa Ligi Kuu ya Soka ya Iran baada ya kuichachafya Naft ya Tehran mabao 2-0 katika uwanja wa Azadi hapa jijini Tehran, siku ya Jumamosi. Katika mchuano huo uliokuwa wa kisisimua wa wiki ya 17 ya Ligi Kuu ya Soka hapa nchini, kiungo Andranik Teymourian aliipa Esteqlal bao la kwanza kunako dakika ya 32. Esteqlal iliendelea kuwa kifua mbele hadi timu mbili hizo zinaenda mapumzikoni. Katika kipindi cha pili, timu hizo zilibanana lakini dakika tatu kabla ya kulia kipenga cha kuhitimisha mchezo, Hanif Omranzadeh alifunga bao safi la kichwa akiunganisha krosi iliyochongwa na Mojtaba Jabbari na kuihakikishia Esteqlal pointi tatu muhimu.
Kwa ushindi huo, Esteqlal inasalia katika nafasi ya kwanza ya msimamo wa ligi ikiwa na pointi 33, ikifuatiwa na Sepahan na Naft ya Tehran ambazo zina pointi 30.
Spoti Afrika
Hatimaye al Shabaab yaruhusu soka lakini kwa masharti
Kundi la wanamgambo wa Somalia la al Shabaab limeruhusu soka kuchezwa nchini humo, lakini limeweka sharti kuwa vazi la suruali ndiyo livaliwe na wachezaji wakati wa mechi. Kundi la al Shabaab lenye misimamo mikali limeruhusu soka kuanza kuchezwa katika eneo la Shabelle ambalo linalidhibiti.
Mechi ya kwanza chini ya amri hiyo ilikuwa wakati FC Sahan ilipochakazwa na Balguray mabao 4-0 wikendi iliyopita chini ya usimamizi wa viongozi wa al Shabaab.
Ni mara ya kwanza baada ya miaka miwili kwa soka kuchezwa katika eneo hilo baada ya kundi hilo kuupiga marufuku mchezo huo kwa madai kwamba, ulikuwa kinyume cha maadili ya dini ya Kiislamu.
Timu zinazoshiriki katika mashindano hayo ni pamoja na Sahan, Bal-Guri, Horseed, Dekedaha, Elman, Sanai, Bulo-Sheikh na FC Nasiib.
Hata hivyo, kundi hilo lilitoa masharti ya kutoruhusu kuandikwa majina ya wasiofuata dini ya Kiislamu kwenye jezi za timu.
Wachezaji wanatakiwa kuvaa suruali na kusimamisha mechi pale inapofika muda wa kuswali.
Ligi Kuu ya Soka ya Uingereza; Gunners yashindwa kutamba mbele ya City
Manchester City siku ya Jumapili walionyesha tena ari na nia yao ya kuwa mabingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza msimu huu, kwa kuisasambua Arsenali goli 1-0. Kufuatia majirani Man United awali kuifunga QPR magoli 2-0, Man City ilifahamu lazima iwike nyumbani na haikupoteza fursa hiyo. Katika dakika ya 53, David Silva alitia kimyani bao hilo ambalo liliitosheleza City kusalia kileleni mwa ligi. Awali, mkwaju mkali wa Mario Balotelli haukuweza kufua dafu, licha ya kuuelekeza vyema mpira wavuni. Sergio Aguero alikuwa na nafasi ya kuongeza idadi ya mabao, lakini mpira wake ulipaa juu mno, huku Pablo Zabaleta naye akigonga mwamba. Lakini Gunners hawawezi kulalamika kwamba hawakupata nafasi ya kufunga mabao, kwani kipa Joe Hart aliweza kuiokoa timu yake kutokana na mikwaju ya Gervinho, Theo Walcott na Aaron Ramsey.
Hadi sasa, Man City inadumisha rekodi ya kutoshindwa katika uwanja wa nyumbani wa Etihad msimu huu, kwa asilimia 100. Kati ya mechi 28 katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita, Man City imeondoka na sare katika mechi mbili tu.
Katika viwanja vingine, Aston Villa ilishindwa magoli 2-0 ilipocheza na Liverpool. Tottenham nayo inashikilia nafasi ya tatu katika Ligi ya Premier, baada ya kuifunga Sunderland bao 1-0.
Jordi Gomez alisawazisha katika dakika 87 na kupunguza kasi ya Chelsea katika juhudi za kufikia kilele cha Ligi Kuu ya Premier na kuiwezesha timu yake ya Wigan kupata pointi muhimu katika kujinusuru kusalia katika ligi.
Kwengineko, Blackburn ilishindwa magoli 2-1 ilipocheza na West Brom wakati Everton ikilazimishwa sare ya 1-1 ilipokutana na Norwich. Fulham ilithibitisha ngome ya Bolton bado ni dhaifu kwa kuwafunga magoli 2-0 kwa kirahisi. Stoke iliishinda Wolves mabao 2-1 huku mechi moja tu wikendi hii ikikosa mabao, ile kati ya Newcastle na Swansea. Barca Watamba tena Kombe la FIFA la Vilabu
Barcelona wameshinda Kombe la Dunia la Shirikisho la Soka Duniani FIFA kwa vilabu baada ya kuicharaza timu ya Santos ya Brazil mabao 4-0 kwenye mchezo wa fainali uliyochezwa nchini Japan. Ushindi huo umeendeleza rekodi nzuri ya klabu hiyo kwa mwaka huu ambapo wao ni mabingwa wa Ligi ya Hispania maarufu kama La Liga. Aidha, Barca wanashikilia ubingwa wa Vilabu vya Ulaya na pia Kombe la Hispania maarufu kama Spanish Super Cup. Mpachika mabao wa timu ya taifa ya Argentina Lionel Messi aliifunga Barca mabao mawili, huku mengine yakiwekwa kimiani na Xavi pamoja na nahodha na kiungo wa zamani wa Arsenal Cesc Fabregas. Ushindi huo unathibitisha kwamba Barcelona inaendelea kusalia timu bora ya kusakata kandanda duniani.
Uislamu na Michezo
Wiki iliyopita, safu hii iliendelea kukutajieni baadhi ya faida zinazopatikana kutokana na mchezo wa kukimbia au kutembea masafa marefu. Katika kutamatisha kuwadondoleeni baadhi ya faida na umuhimu wa mchezo huo, Sheikh Siraj Henricks anasema kuwa, kiafya, kukimbia kunaongeza nguvu na nishati mwilini. Inasemekana kuwa, kukimbia asubuhi kunaupa mwili nishati mchana kutwa na kukimbia nyakati za jioni kunafungua viungo na kumfanya mtu kuwa na usingizi mwanana usiku kucha. Wataalamu wa afya wanasema kuwa, kukimbia kunamfanya mtu ajiamini na kuwa na ari ya kutekeleza vyema mambo yake. Nukta nyingine muhimu kuhusiana na haya ni kuwa, kukimbia au kutembea kwa masafa marefu kunampunguzia mtu msongo wa mawazo na fikra nyingi. Pamoja na faida, umuhimu na nukta zote tulizokudondoleeni katika kipindi cha leo na vipindi vilivyopita, mchezo huo hauna gharama wala kuhitaji maandalizi na ujuzi wowote. Mtu anaweza kukimbia au kutembea kwa masafa anayoweza, popote pale alipo na muda wowote ule.
MIDO LA UKWELI JONAS GERARD MKUDE SASA FITI KABISA, KUINGIA KAMBINI JUMTATU ZENJI SIMBA SC
KIUNGO
wa kimataifa wa Tanzania, Jonas Gerard Mkude ameanza mazoezi mepesi
kuelekea kurejea uwanjani baada ya kupona maumivu ya goti, aliyoyapata
Juni mwaka huu.
Mkude
aliumia akiichezea timu ya taifa, Taifa Stars katika mchezo wa kirafiki
nchini Botswana mjini Gaborone na baada ya vipimo na tiba, akatakiwa
kupumzika kwa wiki sita.
“Nipo
fiti kabisa kwa sasa, nimeanza mazoezi ya viungo chini ya usimamizi wa
Daktari na ninaendelea vizuri,”amesema kiungo huyo wa Simba SC.
Mchezaji
huyo mahiri wa sehemu ya kiungo wa ulinzi, amesema Jumatatu anatarajia
kujiunga na wachezaji wenzake wa Simba SC kambini visiwani Zanzibar.
Atakaporejea,
mtihani wake wa kwanza Mkude utakuwa kujifua kurudi katika kiwango
chake na baada ya hapo amshawishi kocha Mzambia, Patrick Phiri
kumrejesha kwenye kikosi cha kwanza.
Phiri
amerejea Simba SC kipindi ambacho Mkude ni majeruhi, hivyo hajawahi
kufanya naye kazi na tayari amemuamini kiungo mpya Mrundi, Pierre
Kwizera katika nafasi ya kiungo mkabaji.
Lakini
bado mbele ya wana Simba SC, Mkude ndiye mchezaji anayekubalika zaidi
kuzungusha dimba la chini- hivyo kiungo huyo atalazimika kumshawishi na
kocha Phiri akubaliane naye.
Mkude
anaweza kukosa mechi za mwanzo za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara,
ambayo inatarajiwa kuanza Septemba 20, mwaka huu, Simba SC ikifungua
dimba na Coastal Union Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam Septemba 21.
Mabingwa
watetezi, Azam FC wataanza na Polisi Morogoro Uwanja wa Azam Complex,
Chamazi, Dar es Salaam Septemba 20, mwaka huu, wakati Yanga SC
waliomaliza nafasi ya pili wataanza na Mtibwa Sugar Uwanja wa Jamhuri,
Morogoro siku hiyo.
Washindi wa tatu, Mbeya City wataanza na JKT Ruvu ya Pwani, Uwanja wa Sokoine, Mbeya Septemba 20.
Mechi
nyingine za ufunguzi za Ligi Kuu zitakuwa kati ya Stand United
watakaoikaribisha Ndanda ya Mtwara Uwanja wa Kambarage, Shinyanga,
Mgambo JKT wataikaribisha Kagera Sugar Uwanja wa Mkwakwani, Tanga na
Ruvu Shooting watakuwa wenyeji wa Prisons Uwanja wa Mabatini, Mlandizi
mkoani Pwani.
![]() |
Anarudi; Kiungo Jonas Mkude ameanza mazoezi mepesi na Jumatatu anaingia kambini Simba SC |
COUTINHO KUENDELEZA MAKALI YAKE LEO TAIFA?
KIUNGO
mpya wa Yanga SC, Mbrazil Andrey Coutinho aling’ara katika mechi za
kirafiki za timu hiyo visiwani Zanzibar akifunga mabao mawili katika
michezo mitatu.
Na alifunga mabao mazuri Uwanja wa Amaan, Zanzibar moja kila mchezo, Yanga SC ikishinda 2-0 mara zote dhidi ya Shangani na KMKM.
Zaidi
ya kufunga mabao, Coutinho alionyesha uwezo mkubwa mno wa kucheza soka-
kwa ujumla umiliki wa mpira, kasi, utoaji wa pasi, upigaji krosi, kona
na mashuti ya mbali.
Alionyesha
uwezo wa kupasua katikati ya wachezaji wa timu pinzani na kufumua
mashuti ya kushitukiza na kufunga mabao yake hayo mawili mazuri.
Kwa
mashabiki wa Yanga SC wa Dar es Salaam waliosikia sifa za Coutinho
Zanzibar, bila shaka leo itakuwa fursa nzuri kwao kujionea wenyewe juu
ya Mbrazil huyo.
Watapata
fursa hiyo wakati Yanga SC ikimenyana na Thika United ya Kenya katika
mchezo wa kirafiki jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mchezaji
mwingine mpya wa Yanga SC kutoka Brazil, Geilson Santana ‘Jaja’ ambaye
pamoja na kufunga bao pekee katika ushindi wa 1-0 dhidi ya Chipukizi
Uwanja wa Gombani, Pemba hakuvutia sana kiuchezaji, naye atakuwa na
nafasi nyingine ya kudhihirisha uwezo wake kwa wana Yanga wa Dar es
Salaam.
Kwa
ujumla kocha mpya, Mbrazil, Marcio Maximo atahitaji kuendeleza rekodi
ya ushindi baada ya kushinda mechi zote tatu za kujipima nguvu Zanzibar.
![]() |
Kifaa cha ukweli; Andrey Coutinho aling'ara na Yanga SC Zanzibar, je leo ataendelea cheche zake Taifa? |
BEKI MPYA SIMBA SC AWEKEWA PINGAMIZI, WAZENJI WALETA NOMA ILE KONOMA NOMA MSIMBAZI
SAKATA
la usajili wa mchezaji Shafii Hassan aliyesajiliwa na Simba SC kutoka
Zimamoto, limechukua sura mpya baada ya klabu ya Malindi SC kuibuka na
madai kwamba mchezaji huyo ni mali yao.
Katibu
Mkuu wa Malindi Mohammed Masoud Rashid, ameiambia BIN ZUBEIRY leo
kwamba si Zimamoto wala Ashanti United yenye haki ya kumtumia au kumuuza
mwanasoka huyo.
Kwa
hivyo, Malindi ameitahadharisha Simba kutokufanya kosa, na kama
inamtaka beki huyo inalazimika kufanya mawasiliano na uongozi wa timu
hiyo na kufuata taratibu za usajili.
Masoud
alieleza kushangazwa na hatua ya Simba kudai kuwa wamemsajili mchezaji
huyo kutoka Ashanti United, wakati klabu anapaswa kuhamishwa kutoka
Malindi.
Katibu
huyo alidai kuwa, Shafii ana mkataba wa miaka miwili klabu yake ambao
bado haijamalizika, hivyo kitendo cha Ashanti United msimu uliopita
kumsajili, hakikuwa halali.
Masoud
alisema usajili huo ulifanywa kwa mabavu na Chama cha Soka Zanzibar
(ZFA) kwa kushirikiana na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), na
kusisitiza kuwa ni vyema Simba iwasiliane na uongozi wa Malindi yenye
mkataba na mchezaji huyo.
"Tunaitahadharisha
Simba kwamba Shafii ni mchezaji wetu na si wa Zimamoto wala Ashanti.
Ssisi hatutaki ugomvi nao lakini kama hawakuja kumsajili kwetu tupo
tayari kwenda popote kudai haki yetu," alisema Masoud.
Masoud
alidai hiyo si mara ya kwanza Simba kuwatenda kwani walishawahi
kumnyakua kijanja mchezaji wao Adeyoum Saleh, lakini wakawaachia kwa
kuwa hapo mwanzo walikuwa na udugu mzuri.
"Aliposajiliwa
Shafii Ashanti tulipeleka malalamiko ZFA, lakini wakaamua kutupuuza,
hivyo tunaamini alisajiliwa kwa matakwa na maslahi ya viongozi wa ZFA na
TFF kwa kutumia vyeo vyao," alidai.
Katibu
huyo alifika mbali zaidi kwa kutamka wazi kwamba timu ya Zimamoto
inahusika kwa kiasi kikubwa katika kumtorosha mchezaji huyo kwenda
Ashanti, ili waweze kumsajili kirahisi.
"Katika
hili TFF, ZFA, Zimamoto na Ashanti wote walihusika kumtorosha kwani
tulipowasiliana na TFF kipindi hicho walitujibu kuwa hawawezi
kulishughulikia suala hilo," aliongeza.
Akizungumzia
kadhia hiyo, Raisi wa ZFA Ravia Idarous, ameishangaa Malindi, akidai
kuwa wakati wa dirisha dogo msimu uliopita, mchezaji huyo alichezea
Ashanti hadi mwisho wa ligi, lakini klabu hiyo ilikaa kimya.
Alisema
ZFA ilimuidhinisha mchezaji huyo aliyekuwa huru kuichezea Ashanti baada
ya timu hiyo kukamilisha taratibu zote za usajili, na kwamba hafahamu
Malindi inatumia vigezo gani kudai Shafii ni mali yake.
Naye
Katibu wa Zimamoto Ali Jongo akimshangaa Katibu wa Malindi inapata wapi
jeuri ya kudai mchezaji huyo ni wao, na kuongeza kuwa hawana muda wa
kulumbana, bali wanashughulikia mambo mengine yaliyopo mbele yao.
![]() |
Pingamizi; Beki mpya wa Simba SC, Shaffi Hassan akiwa mazoezi na timu yake mpya |
Subscribe to:
Posts (Atom)