Wednesday, 17 September 2014

KURASA ZA MAGAZETI LEO JUMATANO 17/09/2014 KWA HISANI YA MBEYA SPORT.BLOG

Kamakawaida mbeyasport inakupa uhuru wa kujua yaliyo jri leo kwenye magazeti na sio leo tuu nikila siku unakaribishwa kutembelea mtandao huu ilikupata habari za michezo udaku na kurasa za magazeti na habari zinazo tufikia hivi punde .
.

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

TEVEZ BADO MOTO, APIGA ZOTE MBILI JUVE IKIUA 2-0 ULAYA

 MABAO mawili ya mshambuliaji wa zamani wa Manchester United, Muargentina Carlos Tevez usiku huu yameipa ushindi wa 2-0 Juventus ya Italia katika mchezo wa makundi Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Tevez aliyewahi pia kuchezea Manchester City, alifunga bao moja kila kipindi dhidi ya Malmo FF ya Sweden katika dakika za 59 na 90 na kukipa mwanzo mzuri Kibibi Kizee cha Turin katika michuano hiyo mikubwa zaidi ya klabu barani Ulaya.
Wana fainali wa michuano ya msimu uliopita, Atletico Madrid wamepata kipigo cha ugenini kutoka kwa Olympiacos ya Ugiriki cha mabao 3-2.
Mabao ya wenyeji yamefungwa na Arthur Masuaku dakika ya 13, Ibrahim Affelay dakika ya 31 na Mitroglou dakika ya 74 wakati ya wageni yamefungwa na Mario Mandzukic dakika ya 38 na Griezmann dakika ya 87.
Carlos Tevez bado moto, amefunga zote mbili Juve ikiua 2-0 Ulaya

DANNY WELBECK 'ALIVYOWAKERA' ARSENAL JANA...

 MSHAMBULIAJI mpya wa Arsenal, Danny Welbeck jana alikuwa ana nafasi nzuri ya kuwa shujaa wa timu hiyo katika mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Borrusia Dortmund, lakini akashindwa kuitumia.

Mchezaji huyo aliyesajiliwa kwa Pauni Milioni 16 kutoka kwa wapinzani, Manchester United jana alienedelea kupewa nafasi katika kikosi cha kwanza cha The Gunners na kocha Arsene Wenger akionyesha alimsajili kwa sababu alimuamini, lakini akashindwa kuwafurahisha mashabiki.

Haamini macho yake; Mshambuliaji mpya wa Arsenal, Danny Welbeck akiwa amepiga magoti kwa masikitiko baada ya kupoteza nafasi nzuri ya kufunga kipindi cha kwanza jana

Muingereza huyo jana alipata nafasi tatu nzuri za kuifungia Arsenal mabao kuanzia mapema kipindi cha kwanza, lakini zote akashindwa kuzitumia, The Gunners wakichapwa mabao 2-0 na Dortmund ugenini.
Dhahiri Welbeck anahitaji kujiuliza mno baada ya mechi ya jana, kwani iwapo atarudia makosa aliyoyafanya katika mchezo huo, atajitengenezea mazingira ya kuondoka kwenye kikosi cha kwanza Gunners.
Welbeck stumbles at the back post under pressure and misses a chance to give Arsenal the lead
Mshambuliaji wa Arsenal, Danny Welbeck alipata nafasi nzuri ya kufunga hapa bao ambalo lingekuwa la kuongoza kwa Arsenal, lakini akakosa mpira ukimpita namna hii
Nyingine hii; Danny Welbeck akianguka chini na kumshuhudia kipa wa Dortmund, Roman Weidenfeller akienda upande mwingine wa lango na mpira ukitoka nje baada ya kushindwa kuunganishia nyavuni
Welbeck gets into another good shooting position late on but blazes the ball over the bar
Na hii tena; Welbeck akapata nafasi nyingine tena, lakini akapiga juu ya lango

WACHEZAJI MAN UNITED 'WAKESHA' KUANGALIA LIGI YA MABINGWA

 

KLABU ya Manchester United haimo kabia katika michuano ya Ulaya msimu huu baada ya kumaliza nafasi ya saba katika Ligi Kuu ya England msimu uliopita.
Pamoja na hayo, wachezaji wake wameendelea kuonyesha mapenzi na michano hiyo baada ya kukubakli kuchelewa kulala, ili waangalie mechi za Ligi ya Mabingwa. Kipa David de Gea na baadhi ya wachezaji wenzake jana walipoteza muda kwa ajili ya mechi za Ulaya.
Kipa huyo wa kimataifa wa Hispania, ameposti picha akiwa na wachezaji wenzake Marcos Rojo, Rafael, Antonio Valencia, Andreas Pereira, Anderson, Angel di Maria, Ander Herrera na Juan Mata wakipata chakula huku wanaangalia mechi za Ligi ya Mabingwa.
Mzuia michomo huyo wa zamani wa Atletico Madrid ameposti picha hiyo kwenye akaunti yake ya Twitter akiambatanisha na ujumbe: "Chakula cha usiku na timu"!.

Watazamaji; David de Gea akiwa na wachezaji wenzake Marcos Rojo, Rafael, Antonio Valencia, Andreas Pereira, Anderson, Angel di Maria, Ander Herrera na Juan Mata wakipata chakula cha usiku huku wakiangalia Ligi ya Mabingwa

Tuesday, 16 September 2014

Liverpool yarejea katika ligi kuu Ulaya


Liverpool yarejea katika ligi kuu Ulaya
Baada ya miaka 5 nje Liverpool leo wanawakaribisha timu ya Lugorets Razgrad,ya Bulgaria Anflied.
  •  

Wednesday, 3 September 2014

Jumatano, Septemba 3, 2014

     
Leo ni Jumatano tarehe 7 Dhilqaada 1435 Hijria, inayosadifiana na Septemba 3, 2014.
Siku kama ya leo miaka 96 iliyopita, Damascus mji mkongwe na wa kihistoria wa Kiislamu ulikaliwa kwa mabavu na vikosi vya majeshi ya Uingereza. Moja kati ya malengo makuu ya serikali za Ulaya Wakati wa Vita vya Pili vya Dunia ilikuwa kuusambaratisha utawala wa Othmania, lengo ambalo baadaye lilifanikiwa. Wakati utawala wa Othmania ulipokuwa ukisambaratika, maeneo yaliyokuwa chini ya utawala huo moja baada ya jingine yalidhibitiwa na Ufaransa na Uingereza, ambapo mji wa Damascus katika Syria ya leo, pia ulishambuliwa na katika siku kama ya leo ukakaliwa kwa mabavu.
katika siku kama ya leo miaka 71 iliyopita, mkataba wa kusalimu amri Italia katika Vita Vikuu vya Pili vya Dunia ulitiwa saini baina ya wawakilishi wa Italia na nchi waitifaki. Kwa mujibu wa mkataba huo, Waziri Mkuu wa Italia alikubali bila masharti kusalimu amri nchi yake na kwa utaratibu huo, mmoja wa waitifaki muhimu wa Ujerumani ya Kinazi katika vita hivyo, akawa ameondoka katika medani ya vita.
Na miaka 43 iliyopita, yaani tarehe 3 Septemba mwaka 1971, nchi ya Qatar ilipata uhuru toka kwa mkoloni Mwingereza. Katika karne ya 19, Qatar ilikuwa ikihesabiwa kuwa sehemu ya Peninsula ya Kiarabu. Baadaye nchi hiyo ikatawaliwa na kudhibitiwa na Ufalme wa Othmania. Hata hivyo kufuatia kudhoofika utawala huo, Qatar ambayo kuanzia mwaka 1882 na kuendelea kivitendo ilikuwa ikiendeshwa na Uingereza, mwaka 1916 nchi hiyo ya Kiarabu ikawa imetambuliwa rasmi kuwa koloni la Muingereza. Hadi mwaka 1971 Qatar ilikuwa bado inakoloniwa na Uingereza ambapo mwaka huo huo, kwa ushirikiano wa viongozi wa eneo la pambizoni mwa kusini mwa Ghuba ya Uajemi, likaundwa Shirikisho la Umoja wa Falme za Kiarabu. Hata hivyo mnamo Septemba mwaka huo huo, yaani 1971, Qatar ilijiondoa katika Shirikisho la Umoja wa Falme za Kiarabu na kujitangazia uhuru.

Barcelona yaanza LALIGA kwa makeke, Messi ang’ara

     
Timu ya soka ya Barcelona ya Uhispania imeanza msimu mpya wa ligi kuu ya soka nchini humo al-maarufu LALILGA kwa ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya timu ya Elche. Timu hiyo ambao kwa sasa inanolewa na mkufunzi Luis Enrique ikicheza katika uwanja wake wa nyumbani wa Camp Nou ilionekana ikiwa na sura nyingi ngeni baada ya kuwasajili makinda kadhaa akiwemo Munir El Haddadi mwenye umri wa miaka 18 ambaye anaonekana kuwa tishio katika safu ya ushambuliaji. Nyota wa timu hiyo Lionel Messi alipachika mabao 2 katika dakika za 42 na 63, huku bao la tatu likitiwa kimiani na kinda Munir El Haddadi katika dakika ya 46 ya mchezo. Mambo yalionekana yangewavurugikia Barcelona baada ya mlinzi wake Javier Mascherano kulimwa kadi nyekundu katika dakika ya 43 ya kipindi cha kwanza. Hata hivyo pengo la Mascherano halikuwa kikwazo kwa Barcelona kung’ara na kuibuka na ushindi katika mchezo huo. Katika mechi nyingine za ufunguzi zilizochezwa jana Celta de Vigo imeibamiza Getafe mabao 3-1, Villareal imeitandika Levante viboko viwili bila majibu, Granada imeipeleka mchakamchaka  Deportivo de la Coruna kwa kuifunga mabao 2-1, Malaga imeiadhibu Athletic bao 1 kwa yai, huku Sevilla na Valencia zikitoshana nguvu kwa kufungana bao 1-1, matokeoa ambayo yalitawala pia mchezo kati ya Almeria na Espanyol. Ligi hiyo itaendelea tena leo ambapo Real Madrid watamenyamana na Cordoba huku mabingwa watetezi Atletico Madrid wakiwa wageni wa Rayo Vallecano.

Iran yashinda dhahabu, fedha katika Mashindano ya Asia

 

     
Arsalan Amini, mwanaspoti wa Iran amejinyakulia medali 2 za dhahabu katika Mashindano ya Michezo ya Kunyoosha Viungo ya Bara Asia kwa Walemavu maarufu kama Parazurkhaneh, yaliyofanyika nchini Tajikistan. Amini alijishinda dhahabu 2 kwa kunyakua pointi 287 katika mchezo wa kabbade, aina fulani ya mieleka ya makundi iliyochipukia kusini mwa Asia miaka ya 1930. Mchezo huo ulitambulika kimataifa katika Mashindano ya Olimpiki ya Berlin ya mwaka 1936. Mtajikistani Saidmurad Nizomov wa Kundi A aliibuka wa pili kwa kupata pointi 146 na kujishindia medali ya fedha. Medali ya shaba ilimuendea mwanaspoti mwingine wa Tajikistan wa Kundi B, Rahmatullah Aliov, aliyepata pointi 130.
Katika safu ya wanaspoti waliokuwa kwenye viti vya magurudumu katika mchezo huo wa kabadde, Thakur Vinod wa India alishinda dhahabu kwa kupata pointi 206. Muirani Shahabedin Basamtabar aliibuka wa pili kwa kupata pointi 149 na kujishindia medali ya fedha, kando na medali ya dhahabu aliyoishinda hapo awali. Asadullah wa Pakistan aliyeibuka wa tatu alijishindia medali ya shaba kwa kupata pointi 109.
Timu ya Iran imetwaa ubingwa wa mashindano hayo kwa kupata jumla ya pointi 39 ikifuatiwa na Pakistan na Tajikistan zilizopata pointi 33 na 31 mtawalia. India imeboronga katika mashindano hayo na kuvuta mkia.
Wanamichezo kutoka nchi hizo 4 za bara Asia wameshiriki duru ya kwanza ya Mashindano hayo ya Michezo ya Kunyoosha Viungo ya Bara Asia kwa Walemavu maarufu kama Parazurkhaneh yaliyofanyika katika ukumbi wa Abul Qasim Firdaus mjini Dushambe nchini Tajikistan.

Ligi Kuu ya Soka ya Iran
Klabu ya Esteqlal imeendelea kujikita kileleni mwa Ligi Kuu ya Soka ya Iran baada ya kuichachafya Naft ya Tehran mabao 2-0 katika uwanja wa Azadi hapa jijini Tehran, siku ya Jumamosi. Katika mchuano huo uliokuwa wa kisisimua wa wiki ya 17 ya Ligi Kuu ya Soka hapa nchini, kiungo Andranik Teymourian aliipa Esteqlal bao la kwanza kunako dakika ya 32. Esteqlal iliendelea kuwa kifua mbele hadi timu mbili hizo zinaenda mapumzikoni. Katika kipindi cha pili, timu hizo zilibanana lakini dakika tatu kabla ya kulia kipenga cha kuhitimisha mchezo, Hanif Omranzadeh alifunga bao safi la kichwa akiunganisha krosi iliyochongwa na Mojtaba Jabbari na kuihakikishia Esteqlal pointi tatu muhimu.
Kwa ushindi huo, Esteqlal inasalia katika nafasi ya kwanza ya msimamo wa ligi ikiwa na pointi 33, ikifuatiwa na Sepahan na Naft ya Tehran ambazo zina pointi 30.

Spoti Afrika
Hatimaye al Shabaab yaruhusu soka lakini kwa masharti
Kundi la wanamgambo wa Somalia la al Shabaab limeruhusu soka kuchezwa nchini humo, lakini limeweka sharti kuwa vazi la suruali ndiyo livaliwe na wachezaji wakati wa mechi. Kundi la al Shabaab lenye misimamo mikali limeruhusu soka kuanza kuchezwa katika eneo la Shabelle ambalo linalidhibiti.
Mechi ya kwanza chini ya amri hiyo ilikuwa wakati FC Sahan ilipochakazwa na Balguray mabao 4-0 wikendi iliyopita chini ya usimamizi wa viongozi wa al Shabaab.
Ni mara ya kwanza baada ya miaka miwili kwa soka kuchezwa katika eneo hilo baada ya kundi hilo kuupiga marufuku mchezo huo kwa madai kwamba, ulikuwa kinyume cha maadili ya dini ya Kiislamu.
Timu zinazoshiriki katika mashindano hayo ni pamoja na Sahan, Bal-Guri, Horseed, Dekedaha, Elman, Sanai, Bulo-Sheikh na FC Nasiib.
Hata hivyo, kundi hilo lilitoa masharti ya kutoruhusu kuandikwa majina ya wasiofuata dini ya Kiislamu kwenye jezi za timu.
Wachezaji wanatakiwa kuvaa suruali na kusimamisha mechi pale inapofika muda wa kuswali.
Ligi Kuu ya Soka ya Uingereza; Gunners yashindwa kutamba mbele ya City
Manchester City siku ya Jumapili walionyesha tena ari na nia yao ya kuwa mabingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza msimu huu, kwa kuisasambua Arsenali goli 1-0. Kufuatia majirani Man United awali kuifunga QPR magoli 2-0, Man City ilifahamu lazima iwike nyumbani na haikupoteza fursa hiyo. Katika dakika ya 53, David Silva alitia kimyani bao hilo ambalo liliitosheleza City kusalia kileleni mwa ligi. Awali, mkwaju mkali wa Mario Balotelli haukuweza kufua dafu, licha ya kuuelekeza vyema mpira wavuni. Sergio Aguero alikuwa na nafasi ya kuongeza idadi ya mabao, lakini mpira wake ulipaa juu mno, huku Pablo Zabaleta naye akigonga mwamba. Lakini Gunners hawawezi kulalamika kwamba hawakupata nafasi ya kufunga mabao, kwani kipa Joe Hart aliweza kuiokoa timu yake kutokana na mikwaju ya Gervinho, Theo Walcott na Aaron Ramsey.
Hadi sasa, Man City inadumisha rekodi ya kutoshindwa katika uwanja wa nyumbani wa Etihad msimu huu, kwa asilimia 100. Kati ya mechi 28 katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita, Man City imeondoka na sare katika mechi mbili tu.
Katika viwanja vingine, Aston Villa ilishindwa magoli 2-0 ilipocheza na Liverpool. Tottenham nayo inashikilia nafasi ya tatu katika Ligi ya Premier, baada ya kuifunga Sunderland bao 1-0.
Jordi Gomez alisawazisha katika dakika 87 na kupunguza kasi ya Chelsea katika juhudi za kufikia kilele cha Ligi Kuu ya Premier na kuiwezesha timu yake ya Wigan kupata pointi muhimu katika kujinusuru kusalia katika ligi.
Kwengineko, Blackburn ilishindwa magoli 2-1 ilipocheza na West Brom wakati Everton ikilazimishwa sare ya 1-1 ilipokutana na Norwich. Fulham ilithibitisha ngome ya Bolton bado ni dhaifu kwa kuwafunga magoli 2-0 kwa kirahisi. Stoke iliishinda Wolves mabao 2-1 huku mechi moja tu wikendi hii ikikosa mabao, ile kati ya Newcastle na Swansea. Barca Watamba tena Kombe la FIFA la Vilabu
Barcelona wameshinda Kombe la Dunia la Shirikisho la Soka Duniani FIFA kwa vilabu baada ya kuicharaza timu ya Santos ya Brazil mabao 4-0 kwenye mchezo wa fainali uliyochezwa nchini Japan. Ushindi huo umeendeleza rekodi nzuri ya klabu hiyo kwa mwaka huu ambapo wao ni mabingwa wa Ligi ya Hispania maarufu kama La Liga. Aidha, Barca wanashikilia ubingwa wa Vilabu vya Ulaya na pia Kombe la Hispania maarufu kama Spanish Super Cup. Mpachika mabao wa timu ya taifa ya Argentina Lionel Messi aliifunga Barca mabao mawili, huku mengine yakiwekwa kimiani na Xavi pamoja na nahodha na kiungo wa zamani wa Arsenal Cesc Fabregas. Ushindi huo unathibitisha kwamba Barcelona inaendelea kusalia timu bora ya kusakata kandanda duniani.

Uislamu na Michezo
Wiki iliyopita, safu hii iliendelea kukutajieni baadhi ya faida zinazopatikana kutokana na mchezo wa kukimbia au kutembea masafa marefu. Katika kutamatisha kuwadondoleeni baadhi ya faida na umuhimu wa mchezo huo, Sheikh Siraj Henricks anasema kuwa, kiafya, kukimbia kunaongeza nguvu na nishati mwilini. Inasemekana kuwa, kukimbia asubuhi kunaupa mwili nishati mchana kutwa na kukimbia nyakati za jioni kunafungua viungo na kumfanya mtu kuwa na usingizi mwanana usiku kucha. Wataalamu wa afya wanasema kuwa, kukimbia kunamfanya mtu ajiamini na kuwa na ari ya kutekeleza vyema mambo yake. Nukta nyingine muhimu kuhusiana na haya ni kuwa, kukimbia au kutembea kwa masafa marefu kunampunguzia mtu msongo wa mawazo na fikra nyingi. Pamoja na faida, umuhimu na nukta zote tulizokudondoleeni katika kipindi cha leo na vipindi vilivyopita, mchezo huo hauna gharama wala kuhitaji maandalizi na ujuzi wowote. Mtu anaweza kukimbia au kutembea kwa masafa anayoweza, popote pale alipo na muda wowote ule.

MIDO LA UKWELI JONAS GERARD MKUDE SASA FITI KABISA, KUINGIA KAMBINI JUMTATU ZENJI SIMBA SC


KIUNGO wa kimataifa wa Tanzania, Jonas Gerard Mkude ameanza mazoezi mepesi kuelekea kurejea uwanjani baada ya kupona maumivu ya goti, aliyoyapata Juni mwaka huu. Mkude aliumia akiichezea timu ya taifa, Taifa Stars katika mchezo wa kirafiki nchini Botswana mjini Gaborone na baada ya vipimo na tiba, akatakiwa kupumzika kwa wiki sita. “Nipo fiti kabisa kwa sasa, nimeanza mazoezi ya viungo chini ya usimamizi wa Daktari na ninaendelea vizuri,”amesema kiungo huyo wa Simba SC. Mchezaji huyo mahiri wa sehemu ya kiungo wa ulinzi, amesema Jumatatu anatarajia kujiunga na wachezaji wenzake wa Simba SC kambini visiwani Zanzibar. 
Anarudi; Kiungo Jonas Mkude ameanza mazoezi mepesi na Jumatatu anaingia kambini Simba SC
Atakaporejea, mtihani wake wa kwanza Mkude utakuwa kujifua kurudi katika kiwango chake na baada ya hapo amshawishi kocha Mzambia, Patrick Phiri kumrejesha kwenye kikosi cha kwanza. Phiri amerejea Simba SC kipindi ambacho Mkude ni majeruhi, hivyo hajawahi kufanya naye kazi na tayari amemuamini kiungo mpya Mrundi, Pierre Kwizera katika nafasi ya kiungo mkabaji. Lakini bado mbele ya wana Simba SC, Mkude ndiye mchezaji anayekubalika zaidi kuzungusha dimba la chini- hivyo kiungo huyo atalazimika kumshawishi na kocha Phiri akubaliane naye.   Mkude anaweza kukosa mechi za mwanzo za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, ambayo inatarajiwa kuanza Septemba 20, mwaka huu, Simba SC ikifungua dimba na Coastal Union Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam Septemba 21. Mabingwa watetezi, Azam FC wataanza na Polisi Morogoro Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam Septemba 20, mwaka huu, wakati Yanga SC waliomaliza nafasi ya pili wataanza na Mtibwa Sugar Uwanja wa Jamhuri, Morogoro siku hiyo. Washindi wa tatu, Mbeya City wataanza na JKT Ruvu ya Pwani, Uwanja wa Sokoine, Mbeya Septemba 20. Mechi nyingine za ufunguzi za Ligi Kuu zitakuwa kati ya Stand United watakaoikaribisha Ndanda ya Mtwara Uwanja wa Kambarage, Shinyanga, Mgambo JKT wataikaribisha Kagera Sugar Uwanja wa Mkwakwani, Tanga na Ruvu Shooting watakuwa wenyeji wa Prisons Uwanja wa Mabatini, Mlandizi mkoani Pwani.

COUTINHO KUENDELEZA MAKALI YAKE LEO TAIFA?


KIUNGO mpya wa Yanga SC, Mbrazil Andrey Coutinho aling’ara katika mechi za kirafiki za timu hiyo visiwani Zanzibar akifunga mabao mawili katika michezo mitatu. Na alifunga mabao mazuri Uwanja wa Amaan, Zanzibar moja kila mchezo, Yanga SC ikishinda 2-0 mara zote dhidi ya Shangani na KMKM. Zaidi ya kufunga mabao, Coutinho alionyesha uwezo mkubwa mno wa kucheza soka- kwa ujumla umiliki wa mpira, kasi, utoaji wa pasi, upigaji krosi, kona na mashuti ya mbali. Alionyesha uwezo wa kupasua katikati ya wachezaji wa timu pinzani na kufumua mashuti ya kushitukiza na kufunga mabao yake hayo mawili mazuri.
Kifaa cha ukweli; Andrey Coutinho aling'ara na Yanga SC Zanzibar, je leo ataendelea cheche zake Taifa?
Kwa mashabiki wa Yanga SC wa Dar es Salaam waliosikia sifa za Coutinho Zanzibar, bila shaka leo itakuwa fursa nzuri kwao kujionea wenyewe juu ya Mbrazil huyo. Watapata fursa hiyo wakati Yanga SC ikimenyana na Thika United ya Kenya katika mchezo wa kirafiki jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mchezaji mwingine mpya wa Yanga SC kutoka Brazil, Geilson Santana ‘Jaja’ ambaye pamoja na kufunga bao pekee katika ushindi wa 1-0 dhidi ya Chipukizi Uwanja wa Gombani, Pemba hakuvutia sana kiuchezaji, naye atakuwa na nafasi nyingine ya kudhihirisha uwezo wake kwa wana Yanga wa Dar es Salaam.    Kwa ujumla kocha mpya, Mbrazil, Marcio Maximo atahitaji kuendeleza rekodi ya ushindi baada ya kushinda mechi zote tatu za kujipima nguvu Zanzibar.

BEKI MPYA SIMBA SC AWEKEWA PINGAMIZI, WAZENJI WALETA NOMA ILE KONOMA NOMA MSIMBAZI



SAKATA la usajili wa mchezaji Shafii Hassan aliyesajiliwa na Simba SC kutoka Zimamoto, limechukua sura mpya baada ya klabu ya Malindi SC kuibuka na madai kwamba mchezaji huyo ni mali yao. Katibu Mkuu wa Malindi Mohammed Masoud Rashid, ameiambia BIN ZUBEIRY leo kwamba si Zimamoto wala Ashanti United yenye haki ya kumtumia au kumuuza mwanasoka huyo. Kwa hivyo, Malindi ameitahadharisha Simba kutokufanya kosa, na kama inamtaka beki huyo inalazimika kufanya mawasiliano na uongozi wa timu hiyo na kufuata taratibu za usajili.
Pingamizi; Beki mpya wa Simba SC, Shaffi Hassan akiwa mazoezi na timu yake mpya
Masoud alieleza kushangazwa na hatua ya  Simba kudai kuwa wamemsajili mchezaji huyo kutoka Ashanti United, wakati klabu anapaswa kuhamishwa kutoka Malindi. Katibu huyo alidai kuwa, Shafii ana mkataba wa miaka miwili klabu yake ambao bado haijamalizika, hivyo kitendo cha Ashanti United msimu uliopita kumsajili, hakikuwa halali. Masoud alisema usajili huo ulifanywa kwa mabavu na Chama cha Soka Zanzibar (ZFA) kwa kushirikiana na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), na kusisitiza kuwa ni vyema Simba iwasiliane na uongozi wa Malindi yenye mkataba na mchezaji huyo. "Tunaitahadharisha Simba kwamba Shafii ni mchezaji wetu na si wa Zimamoto wala Ashanti. Ssisi hatutaki ugomvi nao lakini kama hawakuja kumsajili kwetu tupo tayari kwenda popote kudai haki yetu," alisema Masoud. Masoud alidai hiyo si mara ya kwanza Simba kuwatenda kwani walishawahi kumnyakua kijanja mchezaji wao Adeyoum Saleh, lakini wakawaachia kwa kuwa hapo mwanzo walikuwa na udugu mzuri. "Aliposajiliwa Shafii Ashanti tulipeleka malalamiko ZFA, lakini wakaamua kutupuuza, hivyo tunaamini alisajiliwa kwa matakwa na maslahi ya viongozi wa ZFA na TFF kwa kutumia vyeo vyao," alidai. Katibu huyo alifika mbali zaidi kwa kutamka wazi kwamba timu ya Zimamoto inahusika kwa kiasi kikubwa katika kumtorosha mchezaji huyo kwenda Ashanti, ili waweze kumsajili kirahisi. "Katika hili TFF, ZFA, Zimamoto na Ashanti wote walihusika kumtorosha kwani tulipowasiliana na TFF kipindi hicho walitujibu kuwa hawawezi kulishughulikia suala hilo," aliongeza. Akizungumzia kadhia hiyo, Raisi wa ZFA Ravia Idarous, ameishangaa Malindi, akidai kuwa wakati wa dirisha dogo msimu uliopita, mchezaji huyo alichezea Ashanti hadi mwisho wa ligi, lakini klabu hiyo ilikaa kimya. Alisema ZFA ilimuidhinisha mchezaji huyo aliyekuwa huru kuichezea Ashanti baada ya timu hiyo kukamilisha taratibu zote za usajili, na kwamba hafahamu Malindi inatumia vigezo gani kudai Shafii ni mali yake. Naye Katibu wa Zimamoto Ali Jongo akimshangaa Katibu wa Malindi inapata wapi jeuri ya kudai mchezaji huyo ni wao, na kuongeza kuwa hawana muda wa kulumbana, bali wanashughulikia mambo mengine yaliyopo mbele yao.